Head image
Govt. Logo

Hits 27035 |  3 online

     
Mkurugenzi Utumishi na Uendeshaji Ndg Juma Ali Simai amewataka maafisa utumishi na wakuu wa vitengo kuendana na kasi ya mabadiliko kwa kufuata sheria kanuni na miongozo ya kazi.
news phpto

Mkurugenzi Utumishi na Uendeshaji Ndg Juma Ali Simai amewataka maafisa utumishi na wakuu wa vitengo kuendana na kasi ya mabadiliko kwa kufuata sheria kanuni na miongozo ya kazi kwa mujibu wa utumishi wa Umma ili kila mtumishi atekeleze majukumu yake ya kazi kwa ufanisi

Mkurugenzi Utumishi na Uendeshaji Ndg Juma Ali Simai amewataka maafisa utumishi na wakuu wa vitengo kuendana na kasi ya mabadiliko kwa kufuata sheria kanuni na miongozo ya kazi kwa mujibu wa utumishi wa Umma ili kila mtumishi atekeleze majukumu yake ya kazi kwa ufanisi

Mkurugenzi Juma ameyasema hayo alipokuwa akiyafungua mafunzo ya tathmini ya upimaji wa mfanyakazi kwa Wakuu wa Divisheni na pamoja na wakuu wa vitengo kwa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Katiba na Sheria kwenye ukumbi wa mkutano wa Wizara ya Katiba na Sheria Mazizini

Ndugu Juma amewataka Wakuu wa Divisheni na pamoja na wakuu wa vitengo hao kufuata taratibu na kuwa waadilifu katika kuwafanyia tathmini wafanyakazi ili kuepuka upendeleo au kumuonea mfanyakazi jambo ambalo litampelekea kukosa haki yake ya msingi

Aidha Mkurugenzi Juma amesema lengo la mafunzo hayo ni kuimarisha Ufanisi wa utekelezaji wa majukumu, kuimarisha utoaji wa huduma bora kwa kufuata utaratibu utakaotumika katika Upimaji Utendaji Kazi kwa Watumishi wa Umma na kuondokana na mfumo wa mazoea ili kuongeza ari ya kiutendaji .

Pia amesisitiza kuwa kila mtumishi anaepatiwa majukumu yake ayatekeze kwa kivitendo ili kufikia dira dhamira na malengo ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuwa na watumishi wenye sifa niwaombe sana mzingatie sheria na kanuni tujitahidi kutenda haki kwa wafanyakazi wote kama anajitahidi na kujituma ipasavyo na mkajiridhisha form ijazwe vizuri na kama maadili na nidhamu mbaya basi kusiwe na upendeleoalisisitiza

Nae muwezeshaji wa mafunzo hayo ndugu Maulid Shaib Ahmada amewataka wakuu wa vitengo kuzingatia mfumo wa Utumishi wa Umma uliowazi na kuwapatia watendaji waliochini yao majukumu yao ya kazi kwa maandishi ili nao waweze kujitathmini badala ya kufanyakazi kwa mazowea.

Maulid amesema mafunzo yanayotolewa juu ya uanzishwaji wa Upimaji Utendaji Kazi yanalenga kuwa na taswira moja ya muundo wa kiutumishi na kupata uwelewa wa pamoja ili kurahisisha utekelezaji bora wa majukumu yao kupitia mfumo huo.

Kuhusu Upandishwaji vyeo katika Utumishi Serikalini Muwezeshaji huyo amesisitiza kuwa utazingatia vigezo maalum ikiwemo misingi yahaki, usawa, uwajibikaji, utendaji mzuri wa kazi, uzoefu na muda wa utangulizi wa kuingia kazini kwa Watumishi wote.

“Kumpandisha Cheo Mtumishi ni sehemu moja wapo ya kumpa motisha kutokana na utendaji wake, kujenga weledi na kuimarisha usimamizi katika Utumishi wa Umma na kwa maana hio upandishwaji vyeo utazingatia kuwepo bajeti iliyoidhinishwa kwa mwaka wa fedha husika, utendaji mzuri, uwajibikaji, heshima, ubunifu, nidhamu, mashirikiano mazuri kati ya Mtumishi na Mtumishi pamoja na Viongozi, sifa za kielimu, uzoefu na maarifa ya kazi aliyonayo katika Daraja alilonalo”

Aidha amesema taratibu za kumpandisha cheo mtumishi ni lazima apimwe utendaji wake wa kazi kwa kujaza fomu ambayo inampandisha Daraja mtumishi husika katika kada husika kutoka Daraja la chini kwenda Daraja la juu kiutendaji na kimaslahi

Fomu ya upimaji utendaji kazi ni Fomu yenye kutoa tathmini ya utendaji wa kazi wa mtumishi baada ya utekelezaji wa majukumu yake kupitia Hati Makubaliano ya utekelezaji wa majukumu ya mtumishi, uwezo na ustadi pamoja na vipimo vya tabia kwa ujumla.

Baada ya kukamilika kwa tathmini ya upimaji wa utendaji kazi ya mtumishi husika na kufanikiwa kupata alama nzuri na kuendelea kwa miaka mitatu (3) mfululizo, tathmin hiyo itamuwezesha mtumishi kuweza kupandishwa cheo, kupatiwa nyongeza ya mishahara na kupewa tuzo, aidha itamuwezesha kushushwa cheo, kupewa barua ya onyo na kutopatiwa

Upimaji utendaji kazi Lazima uwe wazi na wa ushirikishwaji, Ili kupandishwa Cheo italazimika ziwepo ripoti za tathmin za utendaji kazi kwa muda usiopungua miaka mitatu (3) mfululizo zenye alama jumla 65% kwa kila mwakaalisitiza Maulid .

Aidha zoezi la upandishwaji vyeo katika Utumishi wa Umma ni utekelezaji wa maelekezo ya Sera ya Utumishi wa Umma ya mwezi Oktoba, 2010 kama ilivyofafanuliwa katika mkakati wa kisera

Ndugu Maulid amesisitiza suala la mtumishi anapopandishwa cheo kupewa barua ili afahamu stahiki zake kwani cheo kinakwenda sambamba na stahiki bila stahiki mtumishi atakuwa ameongezewa majukumu

Katika risala yao Wakuu wa Divisheni na Wakuu wa vitengo waishukuru Wizara ya Katiba na Sheria kwa kuridhia kufanyika kwa mafunzo hayo ambayo yatatoa fursa kwa kila mshiriki kutekeleza vyema majukumu yake kwa kufuata kanuni na taratibu zote za Kiutumishi .

Jumla ya mada mbili zilizojadiliwa ni upimaji utendaji kazi ambayo imejumuisha maana ya upimaji utendaji kazi, madhumini ya upimaji utendaji kazi,wajibu wa mamlaka husika, hati ya makubaliano, sehemu za hati ya makubaliano, fomu ya upimaji utendaji kazi, sehemu za fomu ya upimaji utendaji kazi

Upandishwaji cheo iliyojumuisha maana ya upandishwaji vyeo, madhumini ya upandishwaji vyeo, dhana ya upandishwaji vyeo, walengwa wa upandishwaji vyeo, vigezo vya upandishwaji vyeo, wajibu wa mamlaka husika katika upandishwaji vyeo, fomu ya upandishwaji vyeo, sehemu za fomu ya upandishwaji vyeo.

Huduma za Tehama

Barua Pepe Msaada wa kisheria

Sisi

Mwanzo Kuhusu Sisi Idara Zetu

Viunga Muhimu

MAHAKAMA DPP WAKFU LRC SADC IKULU

Mawasiliano

Ofisi Kuu
S.L.P 772, Mazizini, Zanzibar
Tel.: +255(24)2234683 Mhe Waziri



Tel.: +255 (24)2234684 Katibu Mkuu,
Fax: +255 (24)2234689
Email: info@sheriasmz.go.tz